Welcome note

Welcome to inspired blog.Be blessed all

Thursday, August 27, 2009

Hivi ulishawahi kujiuliza swali hili!
Ni kwa nini Wakristo wengi hatuoni matunda ya Ukristo wetu,hatufurahii ushindi tulioupata kupitia kwa Yesu Kristo mwamba wa uzima wetu?
Jibu kubwa ni kuwa huwa hatufanyi vitu au mambo yetu ya kiroho kwa kumaanisha!
Mengi tunafanya kwa mazoea na kwa unafiki mkubwa hivyo Mungu anakosa nafasi ya kutusaidia.Tutakapoacha kufanya mambo yetu ya kiroho kwa kubahatisha na Tutakapomruhusu Mungu atawale kweli maisha yetu tutakuwa watu wa tofauti kabisa,tutatembea katika ushindi kila wakati na Mungu wetu atatukuzwa daima.Mimi na wewe basi tuchukue hatua ya kumtegemea Mungu 100%.Kumtegemea yeye 100% maana yake ni kutimiza yale anayotuambia katika Neno lake bila kuwa na wasiwasi wowote ili kwa pamoja tupate kuushiriki utukufu wake aliotuandalia mbinguni,TUMSIFU YESU KRISTO!

No comments:

Post a Comment